Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2018

MAMA SAMIA SULUHU AZINDUA MRADI IRINGA

Picha
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali imedhamiria kuleta mabadiliko ya dhati katika sekta ya utalii kwa kuhakikisha inatanua mtandao wa barabara na pia kuweka mikakati dhabiti ya kuviendeleza vivutio vya utalii viliovyoko kanda ya Kusini ili vichangie ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi. Makamu wa Rais aliyasema hayo leo kwenye hafla ya uzinduzi wa mradi wa kuendeleza utalii kanda ya kusini mwa Tanzania uliofanyika Kihesa Kilolo mkoani Iringa.Makamu wa Rais alisema Serikali imeendelea kuandaa na kutekeleza mipango mikakati mabali mbali kwa lengo la kuhakikisha shughuli za utalii zinasambaa nchi nzima . Makamu wa Rais amasema katika kuendeleza utalii kanda ya kusini, ambapo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea mkopo mwenye masharti nafuu Dola za kimarekani milioni 150 kutoka benki ya Dunia ambapo mradi huo utatekelezwa kwa miaka 6 kuanzia 2017/2018. Mradi huo wenye lengo kuu la kukuza utalii na kipato k...

MSUVA APIGA HAT TRICK NDANI YA BEN AHMED EL ABDI

Picha
Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania Saimon Happygod Msuva usiku wa Jana amelichungulia Mara tatu lango la Benfica ya Guinea Bissau kwenye michuano ya klabu bingwa barani afrika. Ikiwa ni mchezo wa kwanza kwenye mzunguko wa kwanza, Difaa Hassan El Jadida iliibuka na ushindi wa mabao 10-0 katika uwanja wa Ben Ahmed El Abdi mjini El-jadida, Mazghan Morocco, Msuva alifunga magoli yake dakika ya 44,72 na 88.  Mabao mengine ya Difaa Hassan El Jadida yalifungwa na Bakary N'diaye dakika ya nne, Hamid Ahadad dakika za 23, 26, 37, 42 na 47 na Bilal El Magri dakika ya 54. Sasa akina Msuva watakwenda ugenini Guinea Buissau katika mchezo mwepesi kabisa baada ya ushinsi huo mnono wa nyumbani.