WEUSI: TUNATUMIA LUGHA YA KIKUBWA
Kundi la muziki wa hip hop Bongo, Weusi limesema kilichofanyika katika ngoma zao ‘‘Amsha Dude na Nicome’, ni sanaa/lugha ya kikubwa.
Rapper wa kundi hilo Joh Makini amekiambia kipindi cha The Playlist, Times Fm walichofanya katika ngoma hizo mbili ni kucheza na maneno bila kukiuka maadili.
Rapper wa kundi hilo Joh Makini amekiambia kipindi cha The Playlist, Times Fm walichofanya katika ngoma hizo mbili ni kucheza na maneno bila kukiuka maadili.
“Hiyo ni art, sisi tunatumia sanaa, naweza kuongea maneno ambayo kwa lugha nyingine usingeweza kuyatamka kwenye redio lakini kwa sababu natumia sanaa tunaweza jinsi ya kucheza na maneno kufikisha jumbe ambao tunautaka bila kuvunja sheria au kumkwaza mtu yeyote” amesema Joh Makini.
Amsha Dude na Nicome pamoja na Yakulevya ni ngoma ambazo kundi hilo wametoa kwa mwaka huu.
Source; Bongo5
Maoni
Chapisha Maoni