KWASI AANZA KUPIGA TIZI MSIMBAZI LEO ASUBUHI
Beki huyo ambaye alikua akiichezea lipuli amesema anajitambua kama mchezaji wa simba na Leo asubuhi ataungana na wachezaji wenzake kwenye mazoezi ndani ya kambi ya polisi. Licha ya mabosi wake wa wa zamani lipuli wakiendelea kusisitiza kuwa Kwasi bado ni mali yao na watashangaa simba wakimtumia kwa sasa, yeye ameamua kuanza mazoezi na klabu ya simba Leo jumatatu. "Mimi ni mchezaji wa simba baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili na klabu ya simba na suala linalolalamikiwa lishamalizwa na meneja wangu" alisema beki huyo wa kati.