Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

Zimbabwe yajitoa michuano ya CECAFA

Picha
Chama cha mchezo wa soka nchini Zimbabwe (ZIFA) kimetangaza kujitoa katika kombe la michuano ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA ambayo inatarajiwa kuchezwa nchini Kenya kuanzia Desembe 3 hadi 17 mwaka huu. Kupitia mtandao wake wa kijamii ZIFA imesema imeamua kujiengua katika michuano hiyo kufuatia kutotengemaa kwa hali ya kiusalama kwa nchi mwenyeji Kenya. “Kufuatia mashauriano ya kina na wadau wote, Chama cha mchezo wa soka nchini Zimbabwe (ZIFA) kimeadhimia kujitoa katika kushiriki michuano ya CECAFA Chalenji Cup ya mwaka 2017 kutokana nakutotengemaa kwa hali ya kiusalama kwa nchi mwenyeji Kenya, hivyo basi ZIFA imesimamisha maandalizi yote mara moja ya kushiriki kama mgeni mualikwa wa mwaka huu.” Imesema ZIFA “ZIFA inaahidi kujitolea kushiriki katika mashindano yajayo endapo kama hakutakuwa na hali yoyote ya kiashiria cha ukosefu wa usalama. Kujitoa katika mashindano haya si kitu kizuri kwetu, kwa timu, taifa na hata kwa waandaji wa mashindano wenyewe lakini tulihitaji kuf...

Mzimu wa kesi za ukwepaji kodi wazidi kuiandama La Liga, sasa ni zamu ya Modric

Lioneil Messi, Javier Mascherano, Cristiano Ronaldo na Jose Mourinho tayari waliingia matatani katika sheria za nchini Hispania, wote hao walikutwa na kesi inayohusu ukwepaji kodi nchini hapo. Sasa kesi ya namna hiyo imeibuka kwa kiungo wa ushambuliaji wa klabu ya Real Madrid Luca Modric ambaye naye anadaiwa kutenda kosa hilo mwaka 2014 na mamlaka zinazohusiana na kodi za nchini humo zimeanza kumchunguza. Katikati ya mwaka 2013 -2014 Modric alifanga tukio hilo na anadaiwa kukwepa kiasi cha £770,000 ambapo inadaiwa kwamba tukio hilo alilifanya kwa kushirikiana na mkewe Habari za Luka Modric kukwepa kulipa kodi zinakuja masaa machache baada ya mlinzi wa kulia wa Real Madrid Marcelo kupanda kizimbani kujibu kesi kuhusiana na tukio kama hilo. Source:Shaffih Dauda

Ammy Ninje bwana, amfungukia Msuva, Ronaldo awatoa hofu watanzania

Sina shaka jina la Ammy Ninje limejipatia umaarufu mkubwa sana kwa siku za hivi karibuni baada ya kocha huyo kukabidhiwa mikoba rasmi ya kukiongoza kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars kwenye michuano ya Kombe la Chalenji mwezi ujao. Utakua unamfahamu lakini hiki ukifahamu kutoka ndani ya kinywa chake, Ninje hakuibukia tu nje ya mipaka ya bara la Afrika kama ambavyo wengi tunafahamu, bali safari yake ilianzia nchini Afrika Kusini. Alikwenda nchini humo akiwa kama mchezaji baada ya kuambiwa na aliekua kocha wake wakati akiwa kijana mwenye damu inayochemka mwilini kuwa hakua mchezaji tu anaepaswa kuishia ndani ya mipaka ya Tanzania. Baada ya maneno hayo kupasua ngoma za masikio yake, aliitazama miguu yake kisha akapiga konde sehemu ya juu ya kifua chake ambayo ndani yake ndipo ulipojikita moyo wa mwanadamu yeyote yule duniani na hapo ndipo alipoanza safari ya kutafuta mafanikio. Maisha si rahisi bwana, pamoja na changamoto za hapa na pale hatimae Ninje al...

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUUA

Mkazi wa Ipililo wilaya ya Maswa Mkoani Shinyanga, Salum Nkoja (22) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Kisutu akikabiliwa na kosa la mauaji ya kukusudia ya mtu asiyefahamika. Hata hivyo, kwa taarifa zilizoko inadaiwa mshtakiwa huyo alikamatwa na viungo vya binadamu zikiwemo sehemu za siri wanawake. Mshtakiwa alisomewa kosa lake na Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha ambapo amedai mshtakiwa anakabiliwa na kosa moja.

MAHAKAMA YA RUFAA YAMMINYA OSCAR PIOSTOTIUS

Picha
Oscar Pistorius  ameongezewa adhabu ya kifungo kutoka miaka 6 na kuwa miaka 13 na miezi mitano na mahakama ya rufaa nchini Afrika kusini. Pistorius alihukumiwa kwa kosa la kumuua mpenzi wake  Reeva Steenkamp kwa kukusudia. Hatua hii inafuatia madai kutoka upande wa serikali kwamba adhabu aliyopewa awali ya miaka sita ilikuwa ndogo. Pistorius alishtakiwa kumuua mpenzi wake kwa kumpiga risasi 4, katika siku ya wapendanao mwaka 2013, na baadaye Pistorious alisema alifyatua risasi hizo kwa kujua ni mwizi.

MLADIC KUTUMIKIA KIFUNGO CHA MAISHA

Picha
Mladic amepatikana na hatia ya mauaji ya halaiki, uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu. Mauaji haya yalitokana na vita vya miaka ya 90 katika nchi iliyojulikana kama Yugoslavia. Mahakama hiyo imemkuta na hatia kwa makosa 10. Mladic, anayejulikana kama “Chinjachinga wa Bosnia,” ni kiongozi wa mwisho wa kijeshi kukabiliwa na tuhuma za jinai katika mahakama hiyo maalum, iliyowekwa kushughulikia na mauji ya vita vya Bosnia vilivyoshamiri kutoka mwaka 1992 hadi 1995. Mladic, ambaye amekuwa akikabiliwa na mashtaka hayo tangu 2012, ametuhumiwa na makosa ya mauaji ya halaiki 11, jinai za kivita dhidi ya ubindamu kwa madai ya kuhusika kwake kuongoza kampeni ya kuwaua kwa kuvizia kwa risasi watu huko Sarajevo. Mauaji ya 1995 ya zaidi ya Waislam wanaume na wavulana 8,000 huko Srebrenica – mauaji mabaya kuliko yote yaliyowahi kutokea Ulaya tangu Vita vya Dunia II. Waendesha mashtaka katika kesi wameitaka Mahakama ya Kimataifa The Hague (ICT) kumpa adhabu ya kifungo cha mai...

Robinho apewa miaka tisa jela

Picha
MWANASOKA wa zamani wa kimataifa wa Brazil, Robinho ameripotiwa kuhukumiwa kifungo cha miaka tisa jela baada ya kukutwa na hatua ya unyanyasi wa kijinsia. Taarifa nchini Italia zimesema kwambanyota huyo wa zamani wa Manchester City na Real Madrid, kwa pamoja na jamaa wengine watano, walidaiwa kumshambulia binti wa Kialbania katika klabu ya usiku mjini Milan Januari mwaka 2013. Tukio hilo lilitokea wakati mchezaji mwenye umri wa miaka 33 sasa akiwa anachezea AC Milan baada ya kuondoka Etihad mwaka 2010. Source:Bin Zubery

WACHEZAJI WOTE REAL MADRID WAPEWA AUDI MPYA

WACHEZAJI wa Real Madrid wameendelea kufurahia udhamini wa kampuni ya Audi kwa kupewa gari mpya kila mwaka Na baada ya ushindi wa 6-0 Jumanne dhidi ya APOEL mjini Nicosia kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa,  Cristiano Ronaldo  akivunja rekodi yake mwenyewe ya mabao kwenye michuano hiyo wachezaji wote wamepata gari mpya za kisasa. Lakini ni Ronaldo ndiye aliyepewa gari nzuri zaidi ya Audi kuliko wachezaji wenzake. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 alichagua Audi RS7 yenye thamani ya Pauni 150,000. Kocha Zinedine Zidane amepata Audi RS6,Sergio Ramos amechukua Audi R8 Spyder ambayo ni ya gharama zaidi, inayouzwa Pauni 200,000. Nyota wengine wawili, Gareth Bale na Isco wamechukua AudiQ7 Sport, wakati Dani Ceballos na Mateo Kovacic wamechukuaQ7 Sport. Baada ya hapo, wakashiriki mbio maalum za magari ya Audi, Formula E na beki wa kuliaDani Carvajal akaibuka mshindi akifuatiwa na Ramos na Marco Asensio katika nafasi ya pili na ya tatu

Magazeti ya Leo tar 23 Nov 2017

Picha

ICARDI AITENDEA HAKI INTER MILAN

Picha
Mauro Icardi, nahodha wa Inter Milan jana ameifungia timu yake magoli mawili, la kwanza akifunga dakika ya 51 na la pili dakika ya 60 kwenye mechi ya series A uwanja wa Giuseppe Meazza mjini Milan

Yanga mwendo wa goli

YANGA gari limewaka. Kocha Msaidizi wake, Shadrack Nsajingwa ‘Fusso’ amesema wakati wanauanza msimu walikuwa hawatengenezi nafasi nyingi za kufunga, lakini sasa mambo yamejipa.

MUGABE APEWA MASAA KUJIUZULU

Picha
Baada ya kuvuliwa nafasi ya kiongozi wa juu wa Chama cha Zanu- PF Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amepewa masaa tu na Chama hicho kujiuzulu mwenyewe kwenye nafasi ya Urais wa nchi hiyo bila kutumia nguvu. Chama tawala nchini humo leo baada ya kutangaza kuwa kimemvua uongozi Rais huyo mkongwe zaidi barani Afrika, Robert Mugabe, kimemwambia hadi kesho saa 6 mchana awe tayari ametangaza kujiuzulu nafasi ya Urais huku kikimuonya kuwa endapo atakaidi nguvu ya ziada itatumika kumng’oa madarakani. “ Rais wetu wa zamani, Robert Mugabe amepewa muda hadi kesho jumatatu saa 6 mchana awe ameshatangaza kujiuzulu nafasi ya Urais wa Zimbabwe la sivyo nguvu itatumika kumng’oa madarakani .”  chama cha Zanu-PF kimeeleza kwenye ukurasa wao rasmi wa Twitter. Nafasi ya Rais Mugabe itachukuliwa na kiongozi mkuu wa Chama tawala cha Zanu PF aliyechaguliwa leo kwenye kamati kuu ya chama hicho,Emmerson Dambudzo Mnangagwa ambaye pia alishawahi kuwa Makamu wa Rais wa Mugabe kabla ya kutimuliwa
Picha
STRAIKA wa Yanga, Mzambia Obrey Chirwa ameendelea 'kung'ara' katika Ligi Kuu Bara baada ya kufunga 'Hat -trick' yake ya kwanza msimu huu kwenye ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Mbeya City, leo Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Mabao mawili yakifungwa na Emmanuel Martin. Chirwa aliwaamsha mashabiki dakika ya 20 kipindi cha kwanza, Emmanuel Martin naye hakuchelewa akatupia bao la pili dakika ya 23. Na mabao mengine ya chirwa aliyafunga dakika ya 50 na 59 na Emmanuel Martin akafunga dimba kwa kufunga bao la mwisho dakika ya 80.

BOKO AING'ARISHA SIMBA DAKIKA ZA LALA SALAMA

John Boko ameing'arisha simba na kuendelea kuiweka kileleni timu yake kwa kuipatia bao timu yake. Boko alifunga goli hilo kipindi cha pili dakika ya 84, baada ya mabeki wa Tanzania prison kufanya uzembe.  Ushindi wa goli 1-0 umeendelea kuiweka simba kileleni kwa alama 22, azam wakiwa na alama 19, huku mtani wake wa jadi Dar es salaam Yanga African wakiwa na alama 17.

JAJI MKUU: WAHITIMU WA SHERIA WAJIENDELEZE KITAALUMA

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Khamis Juma amewataka wahitimu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kujiendeleza katika fani ya Sheria kwa kuwa na hitaji na hamu ya kujiendeleza zaidi toka kiwango kimoja cha elimu hadi cha juu zaidi. Prof. Juma ameyasema hayo mjini Lushoto katika mahafali ya 17 ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama ambapo wahitimu 150 walitunukiwa Stashahada ya Sheria na wengine 142 walitunukiwa Astashahada ya Sheria. Amesema kwamba wahitimu hao na wasomi wengine wa sheria nchini hawana budi kuzingatia kasi ya sasa ya maendeleo ya dunia na umuhimu wa elimu katika ulimwengu wa leo na kongeza kwa kutokana na hali hiyo ni lazima wajiendeleze zaidi katika fani hiyo. “ Ninawaasa popote pale mtakapokuwa someni na kujiendeeleza na jifunzeni mambo mapya kila siku, karne hii ya 21 ni karne ya teknolojia na habari , ni karne inayowategemea wahitimu wanaojiendeleza na kujifunza kila siku, jiendelezeni hadi kufikia viwango vya juu kulingana na kushindana na yeyote yule dunia...

Michoro ya watoto kutoka Tanzania wazawadiwa Finland.

Picha
Pichani ni watoto waliopata tuzo. Michoro mitatu iliyochorwa na watoto kutoka Tanzania hivi karibuni ilitunukiwa tuzo ya heshima ya vyeti vya stashahada ya maonesho na Taasisi ya Sanaa za watoto na vijana ya Hyvinkää, Finland.Bryton Manyewa(10), Neev Mistry (9) wa shule ya Academic International Primary na Mandela Mtaya (5) wa shule ya chekechea ya Upendo Montessori ndiyo waliofanikiwa kupata tuzo hiyo kwa upande wa Tanzania baada ya kushiriki shindano la michoro liloitwa 'Pamoja' lililotayarishwa na taasisi hiyo ya nchini Finland.

SIMBA YAAHIDI KUIADHIBU PRISON, SOKOINE

Picha
SIMBA SC imeahidi ushindi dhidi ya wenyeji, Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumamosi Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Mratibu wa Simba SC, Abbas Suleiman amesema kwamba kikosi kinaendelea vizuri na maandalizi yake mjini hapa na lengo ni ushindi dhidi ya Prisons. Abbas amesema baada ya wachezaji waliokuwa kwenye           kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilichotoa sare ya 1-1 na wenyeji Benin mjini Cotonou Jumapili kuwasili Jumanne, maandalizi yamepamba moto. Amesema wachezaji wana ari kubwa kuelekea mchezo huo na lengo ni kuendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu baada ya ushindi wa 1-0 katika mchezo wao wa kwanza mjini Mbeya wiki mbili zilizopita dhidi ya Mbeya City. Amesema timu haina majeruhi mpya, ukiondoa wale watatu wa muda mrefu ambao ni kipa Said Mohammed ‘Nduda’ na mabeki Shomari Kapombe na Salim Mbonde. Kwa ujumla baada ya mapumziko ya kupisha mechi za kirafiki za kimataifa zikiwemo za kufuz...

PROF. KITILA AREJEA CCM

Picha
       Chama cha Mapinduzi (CCM) kimemtangaza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Profesa Kitila Mkumbo kuwa amejiunga tena na chama hicho.     Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa chama hicho, Mkoani Singida, Bi. Martha Mlata imesema chama hicho Mkoa wa Singida wanamkaribisha kwa mikono miwili ili waendelee kuimarisha chama katika mkoa huo.    Huku Mlata akielezea jinsi alivyorudi kwenye chama chake cha zamani amesema ni na furaha kuwatangazia wanachama na wapenzi wa CCM Mkoa wa Singida na Tanzania kwa ujuma kuwa, Profesa Kitila Mkumbo amejiunga tena na chama chetu, Ni fursa kubwa kwa mkoa kumpokea mwalimu baada ya kumpoteza mwanafunzi siku chache zilizopita.     Profesa Mkumbo amejiunga wiki moja iliyopita na amelipia ada yote aliyokuwa akidaiwa katika kipindi chote na mimi nilichokifanya ni kuwajulisha tu wanachama wetu kuwa mwana mpotevu karudi nyumbani.

Hatimaye profesa Kapuya atua yanga

Picha
WAZIRI wa zamani wa Michezo nchini, Profesa Juma Othman Kapuya leo amevunja mwiko na kuzuru makao makuu ya klabu ya Yanga, Jangwani mjini Dar es Salaam. Kapuya ambaye ni mpenzi na mwanachama wa klabu ya Simba, ambao ni mahasimu wa Yanga, alifika Jangwani pamoja na jamaa zake kutoka Kaliua, mkoani Tabora. Jamaa hao walisema Waziri kapuya alikwenda kuwatembeza makao makuu ya klabu ya Simba, Mtaa wa Msimbazi, wakati wao ni wapenzi wa Yanga, hivyo wakamshinikiza awafikishe Jangwani. Waziri wa zamani wa Michezo nchini, Profesa Juma Kapuya akiwa makao makuu ya klabu ya Yanga, Jangwani leo mjini Dar es Salaam Walipofika Jangwani, walipokewa na Katibu Mkuu wa klabu, Charles Boniface Mkwasa ambaye alimshikisha Waziri Kapuya Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambalo mara ya mwisho walilitwaa mwaka 2012. Pamoja na hayo, Waziri Kapuya alipata fursa ya kukagua jengo na ofisi mbalimbali za klabu na kupongeza kwa baadhi ya mambo yaliyomvutia .

TIMU 32 ZINAZOELEKEA KOMBE LA DUNIA 2018 ZAKAMILIKA

Peru limekuwa taifa la mwisho kukata tiketi kwenda kushiriki michuano ya kombe la dunia itakayopigwa mwakani nchini Urusi baada ya kuibuka kidedea kwa mabao 2 kwa 0 zidi ya New Zealand. Nini kinafuata ? Baada ya mataifa 32 kufudhu sasa kinachofuatia ni droo ya kupanga timu hizo 32 katika makundi kwa ajili ya fainali hizo, mchezo ambao utafanyika siku ya kesho Ijumaa mjini Moscow. Wababe, Timu za Ubelgiji, Hispania na Uingereza ndio timu ambazo zimefudhu katika michuano hiyo bila kupoteza mchezo hata mmoja na ndio timu pekee ambazo zimeingia katika michuano hiyo kwa kishindo. Timu ya taifa ya Brazil haikuanza vizuri kampeni za kufuzu kwani walishinda mchezo mmoja kati ya sita ya mwanzo lakini baada ya kuja kocha mpya Tite ndipo wakaanza kupata matokeo mazuri wakishinda mechi 10 na kusuluhu 2 kati ya 12. Timu zitapangwa kutokana na viwango vya shirikisho la soka vilivyotangazwa mwezi uliopita, makundi hayo yanatangwazwa kutoka kwenye magroup 4 ambayo tayari yamepatikana baada ya...

MAMIA WAUAGA MWILI WA NDIKUMANA

Picha
Wananchi wa Rwanda pamoja na wapenzi wa soka wa Afrika Mashiriki siku ya jana walipokea kwa mshituko mkubwa kifo cha ghafla cha aliyekuwa kapteni wa timu ya Taifa ya Rwanda, Hamad Ndikumana ambaye pia alikuwa ni mume wa muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Irene Uwoya . Umati wa watu umejitokeza kwenye msikiti wa Qaddafi huko Nyamirambo Rwanda kwa ajili ya kumuaga mwanasoka huyo mkongwe. Ndikumana anadaiwa kufariki dunia mda mchache baada ya kutoka mazoezini akiwa kama kocha was timu ya Rayon sport. Marehemu alikua na mtoto mmoja aliezaa na mwigizaji wa bongo movie Iren uwoya.

Bank ya CRDB yamkabidhi milioni 15 Paul Makonda

Picha
Mkuu was mkoa was dar es salaam Paul makonda amekabidhiwa milioni 15 na bank ya CRDB jijini dar es salaam. Wafanyakazi na wateja wa Benki ya CRDB Dar es Salaam kupitia kwa Mkurugenzi Mtendaji Dr. Charles Kimei leo wamekabidhi msaada wa shilingi milioni 15 kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ili kusaidia ujenzi wa ofisi za Walimu kwa shule za msingi na Sekondari za Dar es salaam. Dr. Kimei alisema msaada huo unatokana na michango ya Wafanyakazi na wateja wa Benki ambao wamehamasika katika kuisaidia serikali kutatua changamoto ya upungufu wa ofisi za walimu Dar es salaam. Pia Dr. Kimei alieleza kwamba hiyo michango ambayo inaendelea kukusanywa na wafanyakazi na matawi ya CRDB ambayo yako 252, na mchango uliokabidhiwa  umetoka makao makuu na tawi Moja la Azikiwe jijini Dar es salaam.

Kibatala aelezea kuhusu hukumu ya Lulu

Picha
Peter Kibatala, wakili wa Elizabeth 'lulu' kupitia akaunti yake ya instegram amefafanua kuhusu hukumu ya lulu kuwa kuna uwezekano was kukata rufaa. Amesema kuwa hakuna hukumu tofauti inayoweza kutolewa kabla mhukukiwa hajatumikia theluthi ya kufungo chake ambacho kwa Lulu itakuwa ni kuanzia miezi mitano. Ndani ya hiyo miezi mitano dhamana inaweza kuombwa wakati wakisubiria rufaaa ianze kusikilizwa. Kwa maana hiyo anaweza kutoka kwa dhamana muda wowote mahakama ikimpatia dhamana. Huwezi kuacha kijana wa miaka 22 mwenye maisha marefu mbele yake ahukumiwe kwa uhalifu kwa sababu ya suala la muda, kwani itaharibu maisha yake ya mbele. Kwa hiyo rufaa imelenga katika kuondoa tatizo hilo. Kukata rufaaa na kuomba dhamana na kufanya kazi za jamii vinaweza kufanyika kwa wakati mmoja wakati suala hili likisubiriwa kusikilizwa na mahakama ya rufaa.

UGANDA WAITAKA SERIKALI KUMKAMATA BASHIR BAADA YA KUWASILI

Picha
Watu wa haki za binadamu wameitaka serikali ya Uganda kumkamata raisi Omar al-Bashr na kumfikisha kwenye mahakama ya ICC.    Wamesema hayo baada ya Bashir kuwasili nchini humo. "We need to arrest this man as directed by ICC. We have a chance today even if we failed in May last year. He has become a social distress. When people see us with him, they will think we don't care about those he killed," Mr Ndifuna said (tunataka kumkamata huyu mtu kama ilivyo takwa na ICC. Tunayo nafasi Leo ata kama tulishindwa mwaka uliopita, amekuwa kikwanzo kwa jamii. Watu watakapo muona pamoja nasi, watazani hatujali kuhusu waliouawa," amesema Bw. Ndifuna

ITALIA NJE KOMBE LA DUNIA

Picha
ITALIA, moja ya mataifa makubwa kisoka itakosekana kwenye Fainali za Kombe la Dunia mwakani kwa mara ya kwanza baada ya miaka 50. Hiyo ni kufuatia kulazimishwa sare ya bila kufungana na Sweden usiku wa jana Uwanja wa San Siro, Milan katika mchezo wa marudiano wa mchujo wa kuwania tiketi ya Urusi 2018. Pia ni huzuni kwa kipa wa kikosi cha italia  Gianluigi Buffon  kwani huu ndo ulikua msimu wake wa mwisho kuichezea timu ya taifa ya italia

TAZAMA VIDEO:Waziri Mpina akiongelea juu ya Uchomaji wa VIFARANGA KUTOKA KENYA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesema serikali ilichoma vifaranga 6,400 kutoka Kenya ili kuzuia magonjwa ya ndege lakini pia mmiliki hakuwa na vibali na vifaranga havikukaguliwa.

JUMA RAIBU: WANAOSEMA NINA KIHEREHRE

Picha
Bombambuzi secretary district Juma Raibu Juma said during his campaign of relational migration to say "Those who say I'm a Fraternity I want to tell you our BAG ward requires a Citizen Leader to Reach and Solve PEOPLE's Problems.